Thursday, August 25, 2011

Mh Jacob Julius ; Afutwa uwaziri rasmi, Mh Uswege asema ana imani na baraza lake, hatishwi wala hatishiki!, Jacob Jaju ajibu mapigo kupitia Facebook

Baada ya aliyekuwa waziri wa protocal / Itifaki Mh Jacob Julius kufutwa rasmi uwaziri kwa kosa la utovu wa nidhamu huku akihusishwa na kuipinga serikali anayoitumikia , hali ya mambo sasa imekuwa vuta nikuvute huku Mh rais Uswege Isaac yeye akisema kuwa ana imani kubwa na mawaziri wake hivyo hatishwi wala hatishiki kamwe.

Huku Mh Uswege akibainisha msimamo wake, naye Bw Jacob Julius amejibu mapigo kupitia mtandao wa facebook huku akitumia jina la Meya Mzumbe katika page ya Mzumbe University, ujumbe huo unasomeka hivi..............
Tanzania inahitaji wapinga rushwa na wapinga matumizi mabaya ya fedha za umma,hao watu hawatashushwa kutoka hewani ni lazima watokee kwenye vyuo vikuu.Sifa ya kupinga matumizi mabaya ya fedha za umma siyo lazima uwe wa chama cha upinzani bali lazima uwe mzalendo.TAZAMENI BUNGE LA TANZANIA LA SASA...
 

No comments:

Post a Comment