Friday, August 26, 2011

Jaju na Uswege tatizo ni Uongozi tu au Kuna Lingine Zaidi?

Pengine kuna bundi ameanza kulia ofisi ya MUSO, ndiyo ni bundi ndiyo maana tunashindwa kuelewa kuna tatizo gani kati ya Jacob Julius na Uswege Isaac ambao wamewahi kufanya kazi pamoja tena nathubutu kusema "ni marafiki wa siku nyingi hawajakutana njiani tu"
Tunashangazwa na vuta nikuvute ya sasa tena kupitia mtandao wa facebook ambapo Bw Jacob Julius anaendeleza mapambano yake aliyoyapachika jina la "WAR AGAINST UFISADI" huku licha ya kuandika kwa mafumbo wenye uzoefu wa maswala ya uandishi tunaelewa kuwa kwa mlango wa nyuma anailenga MUSO lakini kwa mlango wa mbele anamlenga Uswege, kuamini nayosema hebu soma ujumbe huu.............."Meya Mzumbe


Nashauri utaratibu wa kulipana posho zisizo na tija kwa viongozi wa Chuo uondolewe rasmi,huku ndiko tunakojifunzia uwizi na ufisadi.Imagine mtu yupo likizo kwa sasa lakini kila mwisho wa mwezi anapewa posho ya mawasiliano mana ndivyo Bunge ...lilivyobariki,sasa nauliza mtu huyu anawasiliana na nani wakati yupo likizo?HILI NDILO LILILOSABABISHA MAWAZIRI KUMTISHIA USWEGE KWAMBA WATAJIUZULU ENDAPO HATA NIWAJIBISHA,NAMI NIKAMSHAURI ASIWE NA SHAKA YOYOTE MIMI NIKO FLEXIBLE NA HURU HIVYO AAMUE KULINDA MASLAHI YA SERIKALI YAKE,NAYE AKAONA MASLAHI YA SERIKALI YAKE NI KUNIONDOA BARAZANI,NI JAMBO JEMA TENA LA KHERI ILA SASA TUTAHITAJI MJADALA WA WAZI KUJADILI HAYA MAPOSHO WANAYOLIPANA KILA MWISHO WA MWEZI MANA BADO HAIJANIINGIA AKILINI KABISA"
lakini pia soma na ujumbe huu "Meya Mzumbe CCM lazima ianze sasa kupinga uwizi na ufisadi kuanzia kwenye mizizi yaani vyuo vikuu,nikiwa mmoja wa viongozi wastaafu wa CCM Chuo kikuu Mzumbe,sipo tayari kuona chama changu kinakufa na sipo tayari kuona wanaCCM vyuoni tunajifunza kutumia vibaya mali za wanafunzi wenzetu maana kwa kufanya hivyo tunawapa ajenda wapinzani na kuhatarisha ustawi wetu na nguvu yetu kwenye taasisi nyeti kama vyuo vikuu.Jacob Julius(JaJu)"

au soma hapa "
HOJA:wanamzumbe naomba msaada wenu wa kifikra,ni nani anayeweza kukadiria mapato yatokanayo na PRINTER ya MUSO kwa siku?
Plz tafakari kwanza kabla ya kupost koment."
Huo ni ujumbe wa Bw Jacob Julius maarufu kama Jaju katika mtandao wa facebook, sasa sisi hatudhani kama kufutwa uwaziri ndiyo kiini cha haya malumbano, tunataka tuambiwe black and white, kuna nini kati ya watu hawa wawili? tatizo ni uongozi au kuna lililo nyuma ya pazia?



No comments:

Post a Comment