Friday, August 26, 2011

BEAKING NEEEWZ! Banzi Azua Balaa ni baada ya Mrembo Mmoja Wa UDOM kutishia Kujinyonga Akimlilia Rais Huyo Mstaafu Wa MUSO!

Na Reporter wetu Morogoro Mjini,
Habari kutoka chini ya kapeti zinadai kuwa Rais Mstaafu wa MUSO Bw Raphael Banzi ameponea chupuchupu kutinga panapo lupango mara baada ya mrembo mmoja anayesoma chuo kikuu cha Dodoma kutishia kujitia kitanzi akililia penzi la Bw Banzi.
Habari za kina kutoka kwa chanzo chetu ambacho kiko karibu na Banzi kinadai "kweli kaka yule dem kamlilia sana jamaa ila jamaa kabana mpaka mwisho sasa dem alitaka kujinyonga"
Habari zaidi zinaeleza kuwa Bw Banzi ambaye anahusishwa na familia ya kidini yenye Askofu mmoja aliamua kumwekea ngumu mrembo huyo ambaye naye aliona hawezi kuishi bila penzi la Banzi ndipo alipoamua kujipeleka kuzimu kabla ya muda wake kufika , zoezi ambalo hata hivyo liligonga mwamba na mrembo huyo yungali bukheri wa afya.
Mpaka tunakwenda mtamboni hatujafanikiwa kuzungumza na Banzi juu ya taarifa hizi, simu yake haikupatikana kwa zaidi ya mara tatu tulipojaribu kumtafuta.
BLOG HII INATOA POLE KWA BW BANZI KWA MASAIBU HAYO YALIYOMFIKA

No comments:

Post a Comment