Wednesday, September 14, 2011

By Laws Za Banzi Kutupwa Ili Kuengua Wagombea Urais MUSO!

Taarifa za ndani zinafichua mpango wa kuwaengua baadhi ya wagombea urais MUSO mwakani kwa kutupilia mbali kile kinachoitwa "Election by-laws" zilizopitishwa wakati wa Raphael Banzi.

Taarifa kutoka kwa vyanzo vyetu vilivyo karibu na ofisi kuu ya MUSO zinatanabaisha kuwa mpango huo unasukwa mahususi ili kuwashughulikia baadhi ya wale wanaotajwa kuwa na "KIHEREHERE"

Blog hii ina taarifa za uhakika za mpango huo unaoratibiwa kwa kuwashirikisha baadhi ya wabunge ili kutengua election by laws hatua itakayopelekea kurudisha kipengele cha GPA ya 3.5 kwa wagombea urais wa MUSO hatua inayotajwa itawaengua baadhi ya watu wenye azma ya kuwania nafasi hiyo ya urais.
Hatahivyo tayari baadhi ya juhudi za kupinga mpango huo kwa kuwachochea wabunge kuugomea zimeanza huku ikidaiwa ni watu wawili wenye nia ya kugombea wanaoinjinia mpango huo.

Iwe isiwe inatosha kusema kuwa kilele cha yote haya itakuwa ni bunge lijalo la MUSO.

No comments:

Post a Comment