Kile kitendawili cha baadhi ya workshops zinazofanyika Mzumbe University kukosa dhima kiasi cha wadau kuhoji kuwa zina faida gani? au zinamfaidisha nani? sasa kimeteguliwa baada ya Blog hii kujikusanyia ushahidi unaodhihirisha pasi na shaka wa baadhi ya workshops hizo kutumika kujenga mitandao ya kampeni. Blog hii imebaini jambo hili ikiwa ni takribani miezi miwili kabla ya uchaguzi mkuu wa MUSO ambao kadri muda unavyoenda na joto linazidi kupanda kwa kasi. Baadhi ya mbinu zinazotumika kujenga mitandao ya kampeni ni pamoja na wale wenye nia kupata wasaa wa kuzungumza hata kama hawana hoja za msingi lakini pia kumekuwa na tabia ya kukusanya namba za simu za wale wanaosadikiwa kuwa wapiga kura.
Tuesday, November 22, 2011
Breaking Newz; Waziri ataka wanafunzi waandamane kuwadai wenzao waliokopa walipe
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo
Peter Saramba, Arusha NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo amewasihi wanafunzi wa elimu ya juu nchini kuandamana ili kushinikiza waliokopeshwa fedha za elimu miaka ya nyuma walipe ili wapewe wengine. Amesema wahitimu wengi walikopeshwa zaidi ya Sh21 bilioni ili kusoma kwenye vyuo mbalimbali, lakini baada ya kupata kazi wanakwepa kulipa mikopo hiyo. Mlugo alisema wanaosoma vyuoni sasa hawana budi kuandamana ili kuwashinikiza waliotangulia walipe fedha hizo ili ziweze kukopeshwa kwa wanafunzi wengine zaidi.
“Fedha hizo zilikopeshwa kwa wanafunzi wa elimu ya juu tangu utoaji wa mikopo ulipoanza mwaka wa masomo wa 2004/05 na kama zitapatikana zitaiwezesha Serikali kukopesha wahitaji wengi zaidi kuliko idadi ya sasa”, alisisitiza. Naibu Waziri Mulugo alisema hayo alipozungumza kwenye sherehe za mahafali ya Saba ya Chuo Kikuu cha Mount Meru eneo la Ngaramtoni, nje kidogo ya mji wa Arusha. Alisema baadhi ya wanaodaiwa fedha hizi wamefanikiwa kupata ajira rasmi huku wengine wakijiajiri wenyewe baada ya Serikali kugharamia elimu yao kupitia mikopo ambayo sasa hawataki kurejesha. “Tusiandamane (wanafunzi) kudai mikopo kutoka bodi ya mikopo pekee, sasa tuandamane pia kushinikiza waliokopeshwa sasa wanafanya kazi au kujiajiri warejeshe fedha walizokopeshwa ili ziingizwe kwenye mzunguko utakaowezesha wengi kufaidika,” alisema Mulugo akipigiwa makofi. Alisema Serikali ina nia ya dhati kuhakikisha wote wanaofaulu na kupata sifa za kujiunga na elimu ya juu wanapata fursa hiyo bila kujali uwezo kiuchumi wa mhusika, wazazi au walezi wake, lakini lengo hilo linakwamishwa na kipato kidogo na changamoto nyingi zinazohitaji kushughulikiwa na Serikali akitaja uboreshaji wa huduma za afya, miundombinu na huduma zingine za kijamii. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Naibu waziri huyo, idadi ya wanafunzi wa elimu ya juu wanaokopeshwa imekuwa ikiongezeka kila mwaka wa masomo ambapo mwaka 2004/5 , Sh 9.9 bilioni zilitumika kuwakopesha wanafunzi 16,345 kabla ya idadi hiyo kuongezeka hadi kufikia wanafunzi 42,729 mwaka uliofuata. Kuhusu maendeleo katika sekta ya elimu, hasa elimu ya juu, Naibu waziri huyo alisema nchi ilipopata uhuru mwaka 1961 kulikuwa na chuo kikuu kimoja pekee lakini sasa vipo vyuo vikuu na vyuo vikuu vishiriki 41, kati ya hivyo 12 vikiwa vy umma na 29 vya binafsi huku udahili ukiongezeka kutoka wanafunzi 14 kwa wakati huo hadi 155,757 kwa sasa. Katika risala yao kwa mgeni rasmi, wahitimu 414 wa Chuo Kikuu cha Mount Meru waliishauri serikali kuwa pamoja na kuanzisha dawati la mikopo vyuoni, muda umefika wa kufikiria kuanzisha Ofisi za Kanda za Bodi ya Mikopo ili kurahisisha na kuongeza ufanisi kiutendaji.
Chanzo; Gazeti la Mwananchi
ST John Wafanya Mahafali
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akiwa na baadhi ya viongozi wa Chuo Kikuu cha
Mtakatifu Yohana (Saint John's University cha Dodoma katika mhafali ya
chuo hicho Novemba 5,2011. Kushoto kwake ni Mkuu wa Kanisa la Anglikan
nchini linalomiliki chuo hicho, Askofu, Dr. Valentino Mokiwa na kulia
kwake ni Mkuu wa Chuo hicho, Askofu Mstaafu, Dr. Donald Mtetemela.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Habari kwa hisani ya Blog ya wanavyuo Tanzania
Ms Asela Miho The pride of Mlimani
The
Chancellor of University of Dar es Salaam, Ambassador Fulgence Kazaura
(left) gives a reward to Ms Asela Miho (right) who graduated with a BA
degree and was the best overall student during the 4th graduation
ceremony of Dar es Salaam University College of Education (DUCE) on
Saturday. (Photo
by Yusuf Badi)
Monday, November 21, 2011
Mawazo gongana; Zamzam, Frank Mhilu &Lupakisyo Mwambinga
Zamzam anasema..."I appriciate t. Congrats to ministry of informtn, communication and technology. Rais umetendea haki wizara hii."
Lupakisyo Mwambinga anasema..."Huu utaratibu ulioanzishwa sikuhizi Green wa kutenganisha dirisha la watu wa msosi wa buku na dirisha la msosi ambao ni zaid ya buku kwa mtazamo wangu sijaupenda its like ubaguz fulani wa wateja na sisi ni wanafunzi."
Frank Mhilu anasema....ni dhahiri, maji mazito hayabebeki, hata pamba vilevile,...
najiuliza hizi kelele za ufisadi wa muso mwisho wake lini, au tulete dr toka india, nadhani ifikie mahali tuseme basi inatosha, viongozi lazima tuwajibike, wadau tunapaswa pia kuwajibika
safari hii hatuna masihara , tutawajibishana tu.
Sunday, November 20, 2011
Maoni ya Mhariri Leo; Acha Punch, acha Majungu, Lete Hoja Mezani
wabunge wa Mzumbe wakiwa Bungeni
Kwenu Wanamzumbe,Naandika tahariri hii nikiwa na majonzi makubwa kwa jinsi baadhi ya Wanamzumbe wanavyotaka kutuvuruga kwa kile kinachoweza kutafsiriwa kuwa ni "tamaa ya madaraka". Ikiwa takribani ni miezi miwili kabla ya uchaguzi mkuu wa MUSO tayari kampeni za chini kwa chini zimeanza (ingawaje ni kinyume na sheria) nimeshalisema hili siwezi kurudia tena walionisikia wameelewa na ambao hawataki kuelewa wangoje sheria itakapowakumbusha wajibu wao. Leo najitokeza tena kulaani vikali "zengwe" miongoni mwa wanamzumbe.
Hapa neno zengwe ni kuchafuana ambapo kunaweza kutafsiriwa kama kupigana punch na majungu, naam! mapuynch na majungu hayawezi kukubalika hata kidogo. Kama wasomi hatulikubali hili , hatulitaki na tutalilaani milele. Sisi ni wasomi hivyo tutaendelea kusimama katika ukweli ndiyo maana nasema kuwa umefika wakati sasa kwa Wanamzumbe kuanza kujitafakari na kuchukua uamuzi sahihi badala ya kuendelea kukumbatia "siasa za majitaka" Naam! iwe isiwe nitasema ukweli daima, leo nasisitiza kuwa Acha punch, acha majungu, lete hoja mezani!
Wabunge Wanavyoipa heko Mzumbe University
Na Mwandishi wetu Dodoma,
Blog hii imefanikiwa kutua mjini Dodoma na kufahamu mbivu na mbichi kuhusu waheshimiwa wabunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania "kuifagilia" Mzumbe University kwa kile kinachodaiwa mafanikio ya kitaaluma , amani na utulivu wa chuo hiki huku wakichagiza "kwanini vyuo vingine visiige kutoka Mzumbe?"
Kutokana na hali hii, wataalamu wa maswala ya miradi na nertworking katika njanja za maendeleo na ujasiriamali chuoni hapa wanatoa wito kwa chuo kikuu Mzumbe kuitumia fursa hii kufanikisha agenda ya maendeleo huku wakisisitiza kuwa "Mzumbe must market its good reputation"
Katiba ya MUSO yaanza kusakwa kwa udi na uvumba
Onesmo Mpinzile mmoja wa wanasheria mahiri wa Mzumbe
Katika kile kinachoweza kudhaniwa kuwa ni mvutano wa kisheria tayari wadau wameanza kuisaka kwa udi na uvumba katiba ya MUSO ingawaje hawakuwa tayari kuieleza Blog hii nini hasa lengo lao? mfano siku ya jana pekee ni zaidi ya watu watano walifika MUSO office kuisaka katiba hiyo. Kumekuwa na tabia ya watu kuisaka katiba ya MUSO hasa inapofika wakati wa uchaguzi. Friday, November 18, 2011
The Untold Story about Professor Faustine Kamuzora
Do you know that Prof Kamuzora is also an Author? see the elite has number of titles in Economics, Social and Development. With experience of teaching for many years and many years of reading and doing research across the world prof Kamuzora is to be acknowledged as one of the distinguished Tanzanian writer in our times, yes!, Mzumbe University has a lot to be proud but having such elite and an author not only it is pride but also something the young generation ought to copy, read his titles click the link below http://www.kamuzora.co.tz/index.php?option=com_content&view=article&id=47&Itemid=61
Mh Amon Chakushemeire; Kajiuzulu au ameandika barua ya kuomba kujiuzulu?
Mh Chakushemeire akizungumza kwenye baraza la mawaziri
Giza limetanda kufuatia taarifa za kujiuzulu kwa waziri wa Protocal wa MUSO Bw Amon Chakushemeire ambazo zimebaki kuwa "hazieleweki". Blog hii imefatilia kwa undani swala hilo na kubaini kuna uelewa mdogo wa mambo ya utawala miongoni mwa watu wanaoeneza taarifa hiyo kwa maana tunaomba tuweke wazi hapa kuwa alichofanya Mh Chakushemeire ni kuandika barua ya kuomba kujiuzulu kwa aliyemteua(rais) ambaye hata hivyo sheria zinamruhusu kuridhia ombi hilo au kukataa hivyo mpaka sasa bado rais wa MUSO hajatoa uamuzi wake kwa maana nyingine Mh Chakushemeire anapaswa kuendelea kuwajibika mpaka rais atakapotoa uamuzi wake vinginevyo kinachofanyika hapa ni kinyume cha sheria hivyo lazima lipingwe vikali nasi tunakuwa watu wa kwanza kutoa msimamo wetu juu ya hili kuwa HATUKUBALIANI NALO.
Subscribe to:
Posts (Atom)