Wednesday, August 31, 2011

Ugonjwa wa Akili Huu? Uchafu, Kukosa Ustaarabu na Angamizo la Mazingira Yetu!

Hivi kuna nini Mzumbe? tatizo letu nini? ona sasa "upuuzi" wa namna hii msomi wa chuo kikuu Mzumbe anatupa takataka hovyo, ana tatizo la akili? natumia maneno makali ili iwe onyo, sisi tunasema HILI HALIKUBALIKI HATA KIDOGO.

Mzumbe Auditors' Party Umewaona Hao?

Kama Kawaida ya Blog hii siku ya jana Kamera ziliwanasa wakaguzi wa mahesabu na fedha a.k.a Auditors(PSAFI)

wakiwa kiwanja fulani walipoamua kujumuika pamoja kusherehekea Idd El fitri , sasa tufate uone tukio kamili hapa chini.........................!

Hapa wamesahau stargard wanafurahia Idd teh teh teh!
Duuuu! cheki mambo hayo wanacheka tuuu!
Tupo pamojaaaaaa, cheki wanavyofurahi
Mwenyekiti wa PSAFI Mr Danny akitema cheche zake hapa !
Ikumbukwe kuwa wasomi hawa wa PSAFI wamejiwekea historia ya namna yake ya umoja na mshikamano haijawahi tokea tukio la namna hii, ni la kwanza hili, je Faculty nyingine mpo hapo?

Jamaa Alipovamia Idd Pasipo Kualikwa, Akodi Baiskeli na Kanzu, Ilibaki Kidogo Aumbuke, Blog hii Ikamnasa!

Na Reporter Wetu,
Katika kuonyesha kuwa za mwizi ni arobaini, jamaa mmoja ambaye anakawaida ya kuibuka kwenye sherehe pasipo kualikwa ameumbuka vibaya jana baada ya kuingia kwenye "domo la mamba"
Blo hii ilimfatilia jamaa huyo hatua kwa hatua tangu akipanda Hiace mpaka Morogoro mjini ambapo aliingia kwenye nyumba fulani maeneo ya Kihonda kisha akatoka akiwa amevaa kanzu na ghafla akaingia kwenye uchochoro fulani na kukodi baiskeli kisha safari ya "kuzamia "ikaanza.
Alipofika kwenye sherehe hiyo ambayo hakualikwa jamaaa kapaki baiskeli yake na kukaa mkekani ghafla mgawa chakula na vinywaji alipomfikia akataka kuponi, ghafla jamaa akasema kaisahau basi akahojiwa "twambie hata rangi ya kuponi" jamaa akashindwa akapaniki akataka kupigana, muda wote huo mwandishi wetu alikuwa anamfatilia ndipo jamaa kwa hasira akapanda baiskeli yake na kutokomea.

Monday, August 29, 2011

Kuelekea Idd Elfitri; TAMSA Mzumbe Watoa Tamko.....Soma Kwa Undani

     Nova Kambota akiwa na Bw Rajab Semgonja Mkuu wa Habari na Mawasiliano TAMSA

Tukiwa tunaelekea sikukuu ya Idd Elfitri baada ya safari ndefu ya siku 30 ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Blog hii imefanya mahojiano na Tanzania Muslim Students Association(TAMSA) chuo kikuu Mzumbe ambapo Mkuu wa Habari na Mawasiliano wa TAMSA Chuo Kikuu Mzumbe Bw Rajab Semgonja alijibu maswali kadhaa kama ifuatavyo......;


MUSO Link; Baada ya safari ndefu ya siku 30 za kufunga na sasa tukiwa tunahesabu masaa kadhaa kabla ya kusheherekea Idd Elfitri, je una lipi la kusema?

Semgonja; Kwanza shukranzi ziende kwa Mwenyezi Mungu kwa kutuweka salama mpaka hatimaye tumefikia siku hii ambayo tunakaribia kusheherekea siku kuu ya Idd, pia nikiri wazi kuwa muda wote wa Ramadhani umekuwa ni kipindi kizuri kwetu waislamu kujitafakari, kuomba toba, kubadili mwenendo wetu na kumrudia Mwenyezi Mungu mweza wa yote, kwa kifupi ni kipindi ambacho kimetujenga na kutuimarisha kiimani.


MUSO Link; Ikizingatiwa kuwa Mzumbe ni sehemu ya wasomi na zaidi ni vijana pia kuna maswala kama ulevi , uasherati na mengine mengi, je unadhani mwezi wa Ramadhani ulisaidia kupambana na mambo haya kwenye jamii ya Mzumbe?

Semgonja; Ni kweli kabisa ndugu mwandishi kuwa mambo maovu kama hayo yapo, kwa upande mmoja mwezi mtukufu wa Ramadhani umetujenga sana lakini umesaidia baadhi ya watu kubadili mwenendo wao hata hivyo bado hatujafanikiwa kwa asilimia mia moja hivyo mapambano yanaendelea, tutaendelea kuwahimiza wanamzumbe waachane na uovu na kuomba toba kwa Mwenyezi Mungu.


MUSO Link; Kesho ni siku kuu ya Idd , je mmejiandaeje kusherehekea siku hiyo?

Semgonja; Kesho tutakuwa na Baraza la Idd ambapo waislamu tutakusanyika pamoja, kuswali, kupata mawaidha ya walimu,tutasheherekea pamoja na ndugu zetu kutoka Mzumbe secondary na baadhi ya wafanyakazi, sambamba na hayo tutakula pamoja na kupata wasaa mzuri wa kusikiliza nasaha kutoka kwa Maimam na walimu wa Dini yetu, hivyo tunamshukuru Mungu kuwa maandilizi ya siku kuu ya Idd yanaendelea vizuri sana.


MUSO Link; Mwishowe wewe kama kiongozi wa dini na msomi wa chuo kikuu, je nini wito wako kwa waislamu wa Mzumbe na wanamzumbe kwa ujumla?

Semgonja; Kwanza natoa wito kwa waislamu wote kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutufikisha siku hii ya Idd lakini pia natoa wito kwa kuwataka Wanamzumbe wote kila mmoja kwa nafasi yake kujitafakari, kutubu , kuwa na mwenendo mwema unaompendeza Mwenyezi Mungu.


MUSO Link; Asante kwa ushirikiano na Idd Mubarak

Semgonja; Asante ndugu mwandishi nasi kama TAMSA tunakukaribisha kwenye Baraza la Idd

Vita Ya Kumrithi Uswege Sasa Yapamba Moto, Kampeni Zaanza Kimyakimya

Kuna vita ya madaraka imeanza kuelekea uchaguzi mkuu wa MUSO mwakani Blog hii inaripoti bila wasi......

Utafiti wa kina ulioendeshwa na jopo la wanahabari wa Blog hii umebainisha kuwepo kwa kampeni za chini kwa chini za baadhi ya "watu" kuwania urais.
Haijafahamika mara moja iwapo watu hao wanafahamu kuwa wanafanya makosa kuanza kampeni kabla ya muda? taarifa zaidi zinaeleza kuna mikakati mitano inayotumika kufanikisha mbinu hizo;
Kwanza ni "kujichanganya na watu" mbinu hii inafanywa kwa baadhi ya watu wenye nia ya kuwania kujisogeza karibu na watu hususani sehemu ya kula, mbinu ya pili kuvaa vizuri "kulipuka" watu hao wanadaiwa kushona nguo nzuri kiasi kwamba wanataka kujenga picha kuwa wanafaa kukabidhiwa mikoba ya Uswege, mbinu ya tatu ni socialization hawa wanatumia vitu kama mechi za kirafiki kueneza propaganda zao, nne ni kuunda mitandao ya kuratibu kampeni na tano kutumia silaha ya ufaculty.
 Uchunguzi zaidi unawataja wahusika wa mbinu hizi kwa faculty zao(majina tunayahifadhi lakini baadae tutayaanika) , wahusika hao ni pamoja na yule wa social science ambaye huongea kwa upole sana na ni smart kwa mavazi kupindukia, wa pili ni yule wa Laws ambaye ni mcheshi na mwongeaji sana , wa tatu ni yule wa BPA/SOPAM ambaye anapenda kushiriki kwenye midahalo ya hapa na pale na wa nne ni yule wa Commerce ambaye anajenga nertwork yake kimyakimya kwa kushirikisha baadhi ya watu maarufu hapa chuoni.

Blog hii inatoa wito kwa wahusika kuacha vitendo hivyo kwani siyo muda muafaka hivyo ni kinyume cha sheria.

Faculty Of Science&Technology Waja na Mworabaini Wa Matatizo Yao!

Viongozi wa Faculty of Science and Technology
Members wote wa Faculty of Science and Technology wamefanya kikao kinacholenga kuibua changamoto zinazoikabili faculty hiyo na kuja na suluhisho.
Hayo yalisemwa katika kikao kilichofanyika LT2 ambacho kimekuja na maazimio kadhaa yanayolenga kuifanya faculty hiyo kuwa kitovu cha wanasayansi chuo kikuu Mzumbe na Taifa kwa ujumla.

Nova Kambota; Imetosha Naomba Nijibu Hoja Sasa!

Nova Kambota

KWA KUZINGATIA KUWA MZUMBE NI JAMII YA WASOMI NA WANATAALUMA HAITEGEMEWI KUFANYA MAMBO KWA MAZOEA BALI HOJA NA MANTIKI HALIKADHALIKA UNAPOTOKEA UVUMI WOWOTE NI LAZIMA UTOLEWE MAELEZO.
KUFUATIA KUANZISHWA KWA BLOG HII YA KUNA MALALAMIKO KADHAA YAMETOLEWA AMBAYO KAMA WAZIRI WA HABARI WA MUSO NALAZIMIKA KUYATOLEA MAELEZO KAMA IFUATAVYO;
1.KWANZA KABISA BLOG HII NI MALI YA WANAMZUMBE WOTE KWA MAANA NI YA MUSO HIVYO NI MALI YA WANAFUNZI WOTE.
2.NATOA WITO KWA WANAMZUMBE KUWAPUUZA WATU WACHACHE WALIOANZA KUHOJI KWANINI IITWE musolink22 HUKU BAADHI WAKIKOLEZA UZUSHI WAO KUWA ETI MIMI NOVA NIMETIMIZA MIAKA 22 SIKU CHACHE ZILIZOPITA HIVYO KWANINI NIWEKE PERSONAL INTEREST KWENYE MUSO? NAOMBA NIELEZE 22 IMETOKA WAPI? 22 NI JUMLA YA HERUFI ZINAZOUNDA NENO "MZUMBE UNIVERSITY ELITES" UKIHESABU IDADI YA HERUFI UTAPATA 22 HIVYO HAINA UHUSIANO NA UMRI WANGU.
3. KILA MMOJA ANARUHUSIWA KUTOA MAONI AU KUHOJI CHOCHOTE NA HATA KUTUMA PICHA NA HABARI KWA NJIA YA EMAIL NASI TUTAICHAPA BILA UPENDELEO.
MWISHOWE SIHITAJI MALUMBANO KATIKA HILI BALI NATOA WITO WA KILA MMOJA WETU KUTOA MAONI YAKE TUFANYEJE ILI KUZIDI KUIBORESHA BLOG YETU HII?
ASANTENI IMETOLEWA TAREHE 30/08/2011
Nova Kambota(Waziri wa Habari-MUSO)

Sakata la Workshop ya MUEDA larindima tena ngoma bado mbichi kabisa!

Baadhi ya wanafaculty wa science and technology
senetor wa science and technology Mh Abed Ngunike
Katika hali isiyo ya kawaida malalamiko kuhusu workshop iliyofanywa na MUEDA yameibuka tena leo. Hali hiyo imejitokeza wakati wa kikao cha wanafaculty wa Science and Technology usiku wa saa nne kwenye ukumbi wa LT2.
Blog hii ilifanikiwa kunasa baadhi ya malalamiko ya wachangiaji ambao walionyesha kukerwa na workshop hiyo waliyodai ipo chini ya kiwango.

EDWIN SAMSON ;DEMOKRASIA YA UKWELI HURUHUSU UHURU WA MAWAZO


Binadamu wengi huzungumzia uhuru wa mawazo lakini hawajui kuwa hakuna uhuru kamwe hapa duniani,Tulipokuwa katika harakati zetu za kugombea Urais kuna watu walijifanya eti wao ndiyo wamezaliwa kuongoza  wanafunzi wenzao wa hapo chuoni,kuna kundi dogo la watu, nawaita kama watu wakupata ambao  hawajui mbele wala nyuma eti wakadai Edwin ni msaliti ni mtoto wa kihuni hawezi kutuongoza sisi wazeeee wa busara.......................Kuna watu wanadhani uongozi ni sehemu ya kujichotea asali na kusahau dhamana halisi walizonazo wanazotakiwa kuwajibika kwa wananchi.HUU NI UPUUZI ETI WATU WANATIMUANA TIMUANA KISA KAPOSHO.........tulihaidiwa bomba kutoa maziwa,viwanja kuwa kama oldtraford,kila mwanafunzi kuwa na laptop .... sisi wasaliti tulikuwa tunaangalia watu wakikushabikia kumbe ni ndoto za alinacha...nawaambieni kama kuna ufisadi wowote sasa hivi nitawapeleka  MAHAKAMANI, yule mshenzi MSTAAFU tulimuonea huruma ...........JAZENI MATUMBO LAKINI KUMBUKA  JELA YAJA

Chuo Chetu Kinajitosheleza; Mdau Atema Cheche!


futa havard of africa acha mzumbe yenyewe kama motto tafuta nyingine

jamani tuondoleeni hilo nine havard of africa katika jina la chuo chetu mzumbe tuliosoma hapo hatuwahi kuwa na mawazo ya kufananisha chuo chetu na kikingine kwani kinajitosheleza chenyewe na mambo yake,na kinatupa mkate na heshima kote ulimwenguni,sasa nyie vizazi vyipya mmekuja na yenu,msiongerze neno kwa mzumbe.kwanza neno havard mmekosea ni Harvard ,wakija jua mnatumia jina lao watakuja juu,hebu nenda kwa waalimu wa sheria hapo chuoni uliza nenda hata kwa mama opio ni mwanasheria mzuri tu.

Onesmo Mpinzile Atetea Uamuzi Wa Mh Uswege Kumtimua Jacob.......Soma uchambuzi wake wa kisheria

Maamuzi ya Mh Uswege Kisheria

Katika taratibu za kisheria kwa maana ya Both administrative and Constitutional law, Alichokifanya Mh Uswege kinakubalika nisijue kibinadamu! Principle za Ministerial kwa maana ya (Collective na Individual) responsibility Waziri au member yeyote wa cabinet haruhusiwi kupinga jambo au hoja yoyote ya serikali bungeni, anatakiwa kufanya hivyo wakati akiwa kwenye vikao vya Cabinet (Baraza la mawaziri), anatakiwa kuonyesha hali hiyo kwa presiding cabinet chairman amabyo kwa kawaida anaweza kuwa President, Vice president au Prime Minister as the circumstance may be.
Ikiwa jambo hilo au hoja hiyo waziri au member yeyote wa cabinet anaona imeshindikana kukubalika na anaona ina maslahi kwa umma au taifa na imekataliwa kujadiliwa na baraza hilo au imetupiliwa mbali!!...Basi mjumbe huyo wa baraza ataamua kujiudhru uwaziri au ujumbe wa baraza ili ajadili jambo hilo kama mbunge...na katika hali hiyo atakuwa huru kulipinga kwa nguvu zake zote. Kama hatajiudhuru wadhifa huo kwanza na akapinga, sheria inasema kwamba President atatakiwa kumfukuza kazi...Jambo la kumfukuza kazi ni discreationlly (au lipo ndani ya maamuzi ya rais, anaweza kufanya hivyo au asifanye hivyo). Hana obligation (ulazima ) wa kumfuta kazi, n hakuna ulazima wa yeye kufanya hivyo...

Jambo hili si jipya liliwahi kutokea hapa Tanzania na nchi nyngi za jumuiya ya madola, mfano miaka ya 1987-89 Kingunge Ngombale Mwilu wakati akiwa Regional Commissioner, 1993 Mh Augustine Lyatonga Mrema alilazimika kujiudhuru uwaziri kutokana na kutoridhika na maamuzi ya jambo kwenye baraza a mawaziri, Pia angalizo hilo lipo katika katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania, 1977, ambayo inasema 'the Minister shall assume office at the pleasure of the President'.
Hivyo kisheria jambo hilo lipo sahihi nisijue mchango wa Jaju katika baraza la Mh Uswege .

Mpinzile  S. Onesmo
+255714702824
+255785702824
craddleb@yahoo.com
craddletz@gmail.com
Mzumbe University, Bachelor of Laws
Mororogoro Tanzania.

Friday, August 26, 2011

BEAKING NEEEWZ! Banzi Azua Balaa ni baada ya Mrembo Mmoja Wa UDOM kutishia Kujinyonga Akimlilia Rais Huyo Mstaafu Wa MUSO!

Na Reporter wetu Morogoro Mjini,
Habari kutoka chini ya kapeti zinadai kuwa Rais Mstaafu wa MUSO Bw Raphael Banzi ameponea chupuchupu kutinga panapo lupango mara baada ya mrembo mmoja anayesoma chuo kikuu cha Dodoma kutishia kujitia kitanzi akililia penzi la Bw Banzi.
Habari za kina kutoka kwa chanzo chetu ambacho kiko karibu na Banzi kinadai "kweli kaka yule dem kamlilia sana jamaa ila jamaa kabana mpaka mwisho sasa dem alitaka kujinyonga"
Habari zaidi zinaeleza kuwa Bw Banzi ambaye anahusishwa na familia ya kidini yenye Askofu mmoja aliamua kumwekea ngumu mrembo huyo ambaye naye aliona hawezi kuishi bila penzi la Banzi ndipo alipoamua kujipeleka kuzimu kabla ya muda wake kufika , zoezi ambalo hata hivyo liligonga mwamba na mrembo huyo yungali bukheri wa afya.
Mpaka tunakwenda mtamboni hatujafanikiwa kuzungumza na Banzi juu ya taarifa hizi, simu yake haikupatikana kwa zaidi ya mara tatu tulipojaribu kumtafuta.
BLOG HII INATOA POLE KWA BW BANZI KWA MASAIBU HAYO YALIYOMFIKA

Jaju na Uswege tatizo ni Uongozi tu au Kuna Lingine Zaidi?

Pengine kuna bundi ameanza kulia ofisi ya MUSO, ndiyo ni bundi ndiyo maana tunashindwa kuelewa kuna tatizo gani kati ya Jacob Julius na Uswege Isaac ambao wamewahi kufanya kazi pamoja tena nathubutu kusema "ni marafiki wa siku nyingi hawajakutana njiani tu"
Tunashangazwa na vuta nikuvute ya sasa tena kupitia mtandao wa facebook ambapo Bw Jacob Julius anaendeleza mapambano yake aliyoyapachika jina la "WAR AGAINST UFISADI" huku licha ya kuandika kwa mafumbo wenye uzoefu wa maswala ya uandishi tunaelewa kuwa kwa mlango wa nyuma anailenga MUSO lakini kwa mlango wa mbele anamlenga Uswege, kuamini nayosema hebu soma ujumbe huu.............."Meya Mzumbe


Nashauri utaratibu wa kulipana posho zisizo na tija kwa viongozi wa Chuo uondolewe rasmi,huku ndiko tunakojifunzia uwizi na ufisadi.Imagine mtu yupo likizo kwa sasa lakini kila mwisho wa mwezi anapewa posho ya mawasiliano mana ndivyo Bunge ...lilivyobariki,sasa nauliza mtu huyu anawasiliana na nani wakati yupo likizo?HILI NDILO LILILOSABABISHA MAWAZIRI KUMTISHIA USWEGE KWAMBA WATAJIUZULU ENDAPO HATA NIWAJIBISHA,NAMI NIKAMSHAURI ASIWE NA SHAKA YOYOTE MIMI NIKO FLEXIBLE NA HURU HIVYO AAMUE KULINDA MASLAHI YA SERIKALI YAKE,NAYE AKAONA MASLAHI YA SERIKALI YAKE NI KUNIONDOA BARAZANI,NI JAMBO JEMA TENA LA KHERI ILA SASA TUTAHITAJI MJADALA WA WAZI KUJADILI HAYA MAPOSHO WANAYOLIPANA KILA MWISHO WA MWEZI MANA BADO HAIJANIINGIA AKILINI KABISA"
lakini pia soma na ujumbe huu "Meya Mzumbe CCM lazima ianze sasa kupinga uwizi na ufisadi kuanzia kwenye mizizi yaani vyuo vikuu,nikiwa mmoja wa viongozi wastaafu wa CCM Chuo kikuu Mzumbe,sipo tayari kuona chama changu kinakufa na sipo tayari kuona wanaCCM vyuoni tunajifunza kutumia vibaya mali za wanafunzi wenzetu maana kwa kufanya hivyo tunawapa ajenda wapinzani na kuhatarisha ustawi wetu na nguvu yetu kwenye taasisi nyeti kama vyuo vikuu.Jacob Julius(JaJu)"

au soma hapa "
HOJA:wanamzumbe naomba msaada wenu wa kifikra,ni nani anayeweza kukadiria mapato yatokanayo na PRINTER ya MUSO kwa siku?
Plz tafakari kwanza kabla ya kupost koment."
Huo ni ujumbe wa Bw Jacob Julius maarufu kama Jaju katika mtandao wa facebook, sasa sisi hatudhani kama kufutwa uwaziri ndiyo kiini cha haya malumbano, tunataka tuambiwe black and white, kuna nini kati ya watu hawa wawili? tatizo ni uongozi au kuna lililo nyuma ya pazia?



BREAKING NEEWZ! MH HASSAN MASSAWE HOI MAFOMU YAMDODEA MKONONI BAADHI YA MA-CR WADAI POSHO!

Kama ulidhani uongozi wa MUSO ni lele mama a.k.a cha mtoto basi muulize waziri wa afya Mh Hassan Massawe ambaye amekumbwa na kigingi cha kwanza kutoka kwa ma-cr. Habari za uhakika zinadai kuwa waliomtia mkosi Bw Massawe ni maclass representative kutoka faculty of science and technology ambao ni ICTM, POM na A.S

Habari zinadai kuwa Bw Massawe alikuja na idea yake ya kukusanya maoni kuhusu dispensary na huduma za afya ambapo aliandaa fomu na kuwakabidhi ma cr ili watu wajaze ndipo kinyume na mategemeo yake ma cr wa science na technology wametaka posho kwa madai kuwa wapo busy na kusambaza fomu ni kazi nzito, naye Massawe akajibu kwa hasira kuwa MUSO haina pesa na ma cr wamemsusia, mpaka tunaenda mtamboni usiku huu mafomu ya Bw Massawe yamerundikana pale MUSO Office.

Ni Lini Viongozi wa MUSO wataona umuhimu wa Kuhamia Kwenye Ofisi Yenye Hadhi Yao

Pichani juu ni baadhi ya viongozi wa MUSO wakiwa na viongozi wa kitaifa(mawaziri wa serikali ya Tanzania) na picha chini ni ofisi ya MUSO(ambayo haina hadhi)
Kila mwenye kuitakia mema serikali ya wanafunzi chuo kikuu Mzumbe anajihoji ni lini serikali ya Mh Uswege itaona umuhimu wa kuhamia kwenye OFISI ZA MAANA?

Kutana na Gudluck William Kijana Mwenye Vipaji Lukuki

Naam! sasa hapa sijui anaigiza au anaongea huyo ndiyo Gudluck William mbunge wa MUSO mwenye vipaji lukuki, sasa hivi punde nimemdaka akichora picha nzuri sana, ipo siku nitamwomba anisaidie kuchora picha kisha tuziweke hapa mtandaoni

BREAKING NEEWZ Prof Kamuzora Atundikwa Kwenye Group Ya Wakata KIU

Kama unadhani natania basi hayaa...! kwa maana taarifa za utafiti za Blog hii zinaonyesha kuwa group ya facebook ya wakata kiu Mzumbe inatumie picha ya profile hiyo hapo juu ambayo kimsingi ni ya prof Kamuzora, sasa haijajulikana iwapo kamuzora mwenyewe anafahamu hilo au?

Website ya Chuo Kikuu Mzumbe Inahitaji Matengenezo Upya

Website ya chuo kikuu Mzumbe www.mzumbe.ac.tz inahitaji matengenezo makubwa ya haraka, MUSO Link inaripoti bila wasi...

Uchunguzi uliofanywa na blog hii umebaini kuwa website ya chuo kikuu mzumbe haina updates za mara kwa mara, wakizungumza na blog hii baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu Mzumbe wamedai kufadhaishwa sana na udhaifu wa website hiyo huku wakisema wazi kuwa inabidi mabadiliko ya haraka yafanyike ili matokeo yawekwe humo pamoja na taarifa mbalimbali za kila siku.

Kuna Utata Hapa Mawaziri Wamelala Au Wamefumba Macho Tu?

Picha moja maelezo elfu moja, ona mawaziri hawa wa MUSO sijui wamefumba macho au wamelala tu?

Spika wa MUSO Mh Asifiwe Afunguka Rasmi na Kukiri Udhaifu Wa Bunge Analoliongoza, Adai halina Kanuni wa Ulinzi Kila dakika ni Mwongozo wa spika!

Spika wa bunge la wanafunzi chuo kikuu Mzumbe Mh Asifiwe Alinanuswe kwa mara ya kwanza tangu kuteuliwa kwake amejitokeza hadharani na kukiri kuwa Bunge la MUSO ni "zigo zito" kutokana na kuongozwa bila kanuni wala ulinzi hali inamfanya kusimamia kila kitu muda wote.
Alikuwa anazungumza na blog hii mapema leo asubuhi ambapo alitolea mfano tabia ya kelele za wabunge "mwongozo wa spika.....mwongozo wa spika" kelele ambazo amedai ni matokeo ya kukosekana kwa kanuni za bunge.

Hii inakuwa ni mara ya kwanza kwa kiongozi mkubwa kwenye srikali ya MUSO kukiri hadharani udhaifu wa bunge la MUSO.

Thursday, August 25, 2011

Mh Jacob Julius ; Afutwa uwaziri rasmi, Mh Uswege asema ana imani na baraza lake, hatishwi wala hatishiki!, Jacob Jaju ajibu mapigo kupitia Facebook

Baada ya aliyekuwa waziri wa protocal / Itifaki Mh Jacob Julius kufutwa rasmi uwaziri kwa kosa la utovu wa nidhamu huku akihusishwa na kuipinga serikali anayoitumikia , hali ya mambo sasa imekuwa vuta nikuvute huku Mh rais Uswege Isaac yeye akisema kuwa ana imani kubwa na mawaziri wake hivyo hatishwi wala hatishiki kamwe.

Huku Mh Uswege akibainisha msimamo wake, naye Bw Jacob Julius amejibu mapigo kupitia mtandao wa facebook huku akitumia jina la Meya Mzumbe katika page ya Mzumbe University, ujumbe huo unasomeka hivi..............
Tanzania inahitaji wapinga rushwa na wapinga matumizi mabaya ya fedha za umma,hao watu hawatashushwa kutoka hewani ni lazima watokee kwenye vyuo vikuu.Sifa ya kupinga matumizi mabaya ya fedha za umma siyo lazima uwe wa chama cha upinzani bali lazima uwe mzalendo.TAZAMENI BUNGE LA TANZANIA LA SASA...
 

Hotuba ya Waziri wa Fedha; Matumaini Kibao!

Waziri wa fedha wa MUSO Mh Alex Getang'ita akisoma hotuba yake Bungeni

MZUMBE UNIVERSITY STUDENTS ORGANIZATION (MUSO)

MINISTRY OF FINANCE, PLANNING AND INVESTMENT.



HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA GETANG’ITA ALEXANDER NYANCHINI (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2011/2012.

TAREHE 22-08-2011

UTANGULIZI:                               

1. Mheshimiwa spika,naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako tukufu likubali kujadili na kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya serikali ya mwaka wa fedha 2011/2012.Pamoja na hotuba hii yapo majedwali yanayoonyesha makisio ya mapato na matumizi.

2. Mheshimiwa spika, awali ya yote napenda kumpongeza Rais wa serikali ya wanachuo kikuu Mzumbe Mh.Uswege Isaac Mwakabonga, kwa kuchaguliwa kuongoza MUSO akiwa rais wa awamu ya kumi. Aidha ninamshukuru sana mheshimiwa Rais kwa imani kubwa aliyonayo kwangu kwa kunichagua kuongoza wizara kubwa na nyeti, ninamuahidi kuwa sitamuangusha. Pia ninampongeza Mh.Happy Joseph kwa kuchaguliwa kuwa makamu wa rais wa serikali ya wanafunzi chuo kikuu Mzumbe. Vilevile naendelea kutoa pongezi kwa  Mh. Benson Fute (Mb),kwa kuchaguliwa kuwa waziri mkuu wa serikali ya wanafunzi wa chuo kikuu Mzumbe. Natoa ahadi ya kushirikiana naye kwa karibu kama mtendaji mkuu wa serikali katika kuhakikiksha tunatenda yale yote Rais aliyotuamini kwayo.

3.Mheshimiwa spika, napenda kukupongeza wewe binafsi kwa kuchaguliwa kuwa spika, na hivyo kuwa mwanachuo wa kwanza wa shahada ya pili (masters) kuongoza bunge hili tangu chuo hiki kilipopata hadhi ya kuwa chuo kikuu.Kuchaguliwa kwako kunatokana na imani kubwa waliyonayo waheshimiwa wabunge kwa kuzingatia busara zako,uwezo na uzoefu wako.Napenda pia kumpongeza Mh. Suzan Kuzilwa kwa kuchaguliwa kuwa naibu spika,nawapongeza pia mawaziri wenzangu wote pamoja na Naibu mawaziri wote, kwa kuteuliwa kwao na Mh.Rais kushika nyadhifa hizo. Aidha, napenda niwapongeze wabunge wote kwa kuchaguliwa na kuteuliwa kuwawakilisha wanachuo wenzetu katika bunge hili, chombo ambacho maamuzi makuu yanayohusu ustawi wa wanachuo kikuu Mzumbe.

4. Mheshimiwa Spika,naomba kwa namna ya pekee niwashukuru Mh.Mabula R. Mabula,Naibu waziri wizara ya fedha na katibu mkuu wa wizara ya fedha Mh. Nanzia Rajab kwa kazi ngumu waliyofanya katika kuandaa bajeti hii.

5. Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia umuhimu na unyeti wa kazi wanazofanya wawakilishi wa madarasa (CR’S), serikali hii imeonelea ni vyema kuwatia motisha angalau kwa posho kidogo hata za mawasiliano kama kifuta jasho cha kazi nzito wanazozifanya. Hii itakuwa ni serikali ya kwanza tangu chuo hiki kianzishwe, kutoa posho kwa wawakilishi wa madarasa (CR’S). Kulingana na ufinyu wa bajeti yetu, kiasi cha fedha walichotengewa si kikubwa sana lakini ni mwanzo mzuri ambao ninaamini kama serikali zijazo zikiufuata na kuuboresha utaleta tija katika ufanisi wa kazi za hawa waheshimiwa.

6.Mheshimiwa Spika, kwa kipindi kirefu chuo kikuu Mzumbe, kimekuwa kikijiweka kando na masuala ya kitaifa ambayo tumekuwa tukiona vyuo vingine vikijihusisha siku hadi siku, serikali hii imejikita sana katika kuwawezesha wana wanachuo kikuu Mzumbe kushiriki katika masuala ya kitaifa na serikali imejipanga kuhakikisha inafanikisha adhima hii ikishirikiana na menejimenti ya chuo ya chuo kikuu Mzumbe.

7. Mheshimiwa Spika, katika bajeti hii serikali imeweka kipaumbele kuiboresha tovuti, ya MUSO ambayo hadi sasa  iko katika hali nzuri, napenda kumpongeza mheshimiwa Waziri husika kwa kazi nzuri anayoifanya.

8. Mheshimiwa Spika,ninayo furaha pia kusimama hapa mbele ili kutoa matazamio ya serikali kwa upande wa mapato na matumizi kwa kipindi cha mwaka mmoja wa madaraka. Bajeti ninayokwenda kuisoma punde imeangalia nyanja zote muhimu kwa maslahi ya wanafunzi wote wa chuo kikuu Mzumbe na hivyo napenda kutanguliza ombi langu kwa waheshimiwa wabunge kuwa makini sana kuchangia kwa mawazo ya kujenga na hatimaye kuipitisha ili wanafunzi wenzetu ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakilalamika kutoona matunda ya pesa zao, kupitia bajeti hii, sasa wakapate kuona matunda hayo.

Naomba nichukue fursa hii sasa niweze kusoma makadirio ya mapato na matumizi ya serikali ya chuo kikuu Mzumbe kwa mwaka wa fedha 2011/2012 kwa kuzingatia mchanganuo wa kila wizara.







MHESHIMIWA SPIKA NAOMBA KUTOA HOJA.

TANZIA MZUMBE UNIVERSITY PROF NJUNWA AAGA DUNIA

BLOG HII NA WANAFUNZI WOTE WA CHUO KIKUU MZUMBE WANAYO HUZUNI KUBWA KUPOKEA TAARIFA ZA MAJONZI KUFUATIA KUFARIKI DUNIA KWA MSOMI NA MWANATAALUMA PROFESSOR MUJWAHUZI NJUNWA ALIYEAGA DUNIA KWA UGONJWA WA KISUKARI SIKU YA JANA. PROF NJUNWA ATAKUMBUKWA KWA MCHANGO WAKE MKUBWA KATIKA SCHOOL OF PUBLIC ADMINISTRATION CHUO KIKUU MZUMBE...............BWANA ALITOA, NA BWANA AMETWAA, JINA LAKE LIHIMIDIWE,NA MUNGU AILAZE PEMA ROHO YA MAREHEMU...AMEN!

Mh Ridhia ; Another Iron Lady, Aweka Rekodi ya kuwa Mbunge wa Kike wa Mwisho kutoka Bungeni, Mwashibanda Aongoza zoezi la kumchangia

Umewahi kumwona huyo dada hapo pichani? mwangalie vizuri tuuuuu, huyo ni Iron Lady Ridhia, ambaye ameweka rekodi ya kuwa mbunge mwanamke kutoka bungeni mnamo saa nane usiku, ndipo Mh Mwashibanda akaongoza harembee ya kumpongeza kwa kumchangia pesa za pongezi, naam! huyo ndiyo Iron Lady Ridhia

Wabunge walimchachafya spika akashindwa kunywa soda yake





Katika kile kinachoonekana kuzidiwa na rabrasha za wabunge inaelezwa kuwa spika alishindwa kunywa soda yake kama anavyoonekana pichani, mpaka BUNGE linaisha Mh huyo hakuweza kuinywa soda hiyo, na hata tulipombana atueleze sababu za kushindwa kunywa soda hiyo yeye aliishia kucheka hatua inayozidi kushawishi kuwa kuongoza bunge si lelemama

Engineer mkuu wa Blog ya MUSO , viva Nova Kambota....!!

Huyu ni Nova Kambota waziri wa mawasilianona Engineer mkuu wa MUSO link akitake note Bungeni, anachukua hoja hapa! heko Nova viva Nova

Mh Temba ; Sauti Ya Upole Hoja Nzito

Kama ulikuwa hufahamu Mh Uswege hajui kuteua mawaziri basi umekosea, nasema hesabu maumivu, je unamfahamu Mh Temba mwone pichani, anasifika kwa kuzungumza kwa sauti ya upole lakini yenye hoja nzito kama sio ujumbe mkubwa.

Unawajua Maveteran wa Siasa za Mzumbe?

Mh Benson Futte waziri mkuu naye yupo kwenye list ya maveteran

Mkongwe Frank Mushi naye ni veteran pia
Vijana wa kazi hawa wabunge hai bungeni wana changamoto za kuitikisa serikali
Wengine hao ni maveteran pia ni wakongwe katika anga za Mzumbe University

Mwashibanda Eloish Mwashibanda na maamuzi magumu

Mh Mwashibanda ameonyesha msimamo wake mara kadhaa bungeni mara baada ya kunukuliwa akianika msimamo wake hadharani, mwone hapa kwenye picha alikuwa akichangia.

Spika wa bunge anawaapisha wabunge wapya mara baada ya Mh Mwashibanda kuchangia juu ya uhalali wa baadhi ya wabunge
Hapa Mwashibanda akanena "Jacob is the great person at Mzumbe lakini kama asipofukuzwa mpaka kesho saa nne mimi pia najiuzulu"
Spika akiendelea na shughuli za bungeni mara baada ya Mwashibanda kuchangia
Baadhi ya makatibu wakifurahia hoja za Mwashibanda ndani ya bunge

Wasemavyo Watani kuhusu Mh Uswge na Mawaziri Wake

Mhh! Mh Kamana unawaza nini? au swaumu kali mkuu..........


Ninyi mawziri wangu mimi nawasikiliza saaana jamani mnanifurahisha sana aisee ila ................!
Mh Uswege nasema hiviiiii...embu nisikilize kwanza............!



Tupo makini tunasikiliza tunafatilia ila aaah! hii stagered itatuua aisee...!

Hivi nyinyi mnavyoniona mkimya mnadhani sijui kubishana eenh! sasa ngojeni niwaoneshe...!

Cabinet Meeting; Ni Hoja Kwenda Mbele

Hii ni picha iliyonaswa na kamera zetu wakati kikao cha baraza la mawaziri kikiendelea, inaelezwa kuwa hapa mawaziri walikuwa wanajiandaa kupeleka bajeti bungeni.