Kwako Rais Jakaya Kikwete,

Ni hivi punde mdogo wangu ambaye amechaguliwa kujiunga na chuo kikuu Mzumbe amenipigia simu na kunieleza jinsi management ya chuo kikuu Mzumbe wakiongozwa na Prof Kuzilwa na Prof Kamuzora jinsi wanavyosuka mgomo kwa lazima. Tuhuma hizi zinachochewa na kitendo cha chuo hiko kwa kushirikiana na TCU kujaza maelfu ya wanafunzi kushinda uwezo wa chuo kiasi kwamba sasa "kuna vuta nikuvute kwenye maswala ya accomodation"

Mpaka sasa inaelezwa kuwa historia ya kutogoma ya chuo kikuu Mzumbe ambayo JK amekuwa akijivunia huenda ikafutika muda wowote kutoka hivi sasa kutokana na tishio la mgomo huo ambao yaelezwa muda wowote waweza kuanza.

Hapa ndipo nataka kumuuliza JK kuwa yeye kama rais haoni kuwa anahujumiwa na maprofessor hawa? je Jk yupo tayari Mzumbe kugeuka "Mlimani?"
  SOMA HABARI KAMILI BOFYA HAPA;http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/185951-mgomo-umeiva-mzumbe-university-jk-unahujumiwa.html