Tuesday, November 22, 2011

Workshops zatumika kama forums za kampeni, siri yafichuka , wenye nia watumia kujitangaza

 Kile kitendawili cha baadhi ya workshops zinazofanyika Mzumbe University kukosa dhima kiasi cha wadau kuhoji kuwa zina faida gani? au zinamfaidisha nani? sasa kimeteguliwa baada ya Blog hii kujikusanyia ushahidi unaodhihirisha pasi na shaka wa baadhi ya workshops hizo kutumika kujenga mitandao ya kampeni. Blog hii imebaini jambo hili ikiwa ni takribani miezi miwili kabla ya uchaguzi mkuu wa MUSO ambao kadri muda unavyoenda na joto linazidi kupanda kwa kasi. Baadhi ya mbinu zinazotumika kujenga mitandao ya kampeni ni pamoja na wale wenye nia kupata wasaa wa kuzungumza hata kama hawana hoja za msingi lakini pia kumekuwa na tabia ya kukusanya namba za simu za wale wanaosadikiwa kuwa wapiga kura.

No comments:

Post a Comment