Sunday, November 20, 2011

Maoni ya Mhariri Leo; Acha Punch, acha Majungu, Lete Hoja Mezani

wabunge wa Mzumbe wakiwa Bungeni
Kwenu Wanamzumbe,
Naandika tahariri hii nikiwa na majonzi makubwa kwa jinsi baadhi ya Wanamzumbe wanavyotaka kutuvuruga kwa kile kinachoweza kutafsiriwa kuwa ni "tamaa ya madaraka". Ikiwa takribani ni miezi miwili kabla ya uchaguzi mkuu wa MUSO tayari kampeni za chini kwa chini zimeanza (ingawaje ni kinyume na sheria) nimeshalisema hili siwezi kurudia tena walionisikia wameelewa na ambao hawataki kuelewa wangoje sheria itakapowakumbusha wajibu wao. Leo najitokeza tena kulaani vikali "zengwe" miongoni mwa wanamzumbe.

Hapa neno zengwe ni kuchafuana ambapo kunaweza kutafsiriwa kama kupigana punch na majungu, naam! mapuynch na majungu hayawezi kukubalika hata kidogo. Kama wasomi hatulikubali hili , hatulitaki na tutalilaani milele. Sisi ni wasomi hivyo tutaendelea kusimama katika ukweli ndiyo maana nasema kuwa umefika wakati sasa kwa Wanamzumbe kuanza kujitafakari na kuchukua uamuzi sahihi badala ya kuendelea kukumbatia "siasa za majitaka" Naam! iwe isiwe nitasema ukweli daima, leo nasisitiza kuwa Acha punch, acha majungu, lete hoja mezani!

No comments:

Post a Comment