Monday, December 5, 2011

Office Mpya Ya MUSO na Vita Ya Madaraka Mzumbe University



Office Mpya ya Serikali ya Wanafunzi Mzumbe imedaiwa kugeuka source ya mvutano miongoni mwa Wanamzumbe wenye lengo la kuwania urais. Habari za kina ambazo Blog hii inazo ni juu ya uwepo wa mpambano mkali miongoni mwa Wanamzumbe kugombea kukaa ndani ya ofisi hiyo.

Nchimbi ala NONDOZ ya PHD Mzumbe University


Waziri wa michezo na habari, Dkr Emmanuel Nchimba (katikati) akiteta jambo na Dkr Lushakuli Saimon kushoto na Dkr Nangawe Abbi kushoto wakati wa mahafali ya 10 ya chuo kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro ambapo Dkr Nchimbi alitunukiwa utafiti wa dhima ya mikopo midogo midogo katika kupunguza umaskini (PHD) wakati Dkr Saimon akitunukiwa utafiti katika ubora wa vituo vya magari ya abiria vya ubungo Dar es Salaam na Msamvu Morogoro huku Dkr Abbi utafiti wa ushirika wa makampuni binafsi katika masoko ya mitaji yanayojitokeza aliofanya masoko ya mitaji Tanzania ambapo jumla watafiti saba walitunukiwa utafiti wa aina mbalimbali (PHD) katika chuo hicho mkoani hapa(Juma Mtanda Blog)

Jaji Samatta Kutunuku Wahitimu 2220 Mzumbe University; Gazeti la Habari Leo


MKUU wa Chuo Kikuu Mzumbe, Jaji Mkuu mstaafu Barnabas Samatta jana alitarajiwa kuwatunuku wahitimu 2,220 wa shahada mbalimbali.

Miongoni mwa wahitimu hao kwenye mahafali ya 10 ya chuo hicho mjini Morogoro wamo saba wa Shahada za Uzamivu (PhD).

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari juzi, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa chuo hicho, Rainfrida Ngatunga alisema miongoni mwa wahitimu saba wa Shahada ya Uzamivu ni Waziri wa Habari, Vijana, Michezo na Utamaduni, Dk. Emmanuel Nchimbi.

Wengine ni Gustav Kunkuta, Simon Lushakuzi, Sunday Makama kutoka Nigeria, George Makoma, Anarabbi Nangawe na Fred Rwechengula.

“Sisi kama chuo (Mzumbe) tunajivunia sana kuona namna uwiano wa jinsia kwa wahitimu unavyoshabihiana kwani kati ya wahitimu wote 1,282 wanaume na 938 wanawake,” alisema Ngatunga na kuongeza kuwa mahafali hayo yalitanguliwa na warsha chuoni hapo juzi.

Miongoni mwa mambo yaliyotarajiwa kufanywa juzi kwenye warsha ni kutambua michango mbalimbali ya wanazuoni waliofanya vizuri kwenye masomo na utafiti.

“Chuo chetu kitachukua fursa hiyo pia kutambua mchango wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa
(NHIF) katika ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike kwenye Kampasi Kuu Morogoro,” aliongeza.

Ngatunga alisema chuo pia kinatambua mchango mkubwa na uungaji mkono wa Benki ya CRDB katika mchakato mzima wa kuandaa kongamano la wadau wa elimu la chuo hicho lililofanyika Mei mwaka huu.

Akifafanua zaidi kuhusu mahafali hayo, Ngatunga alisema miongoni mwa wahitimu hao 1,365
watatunukiwa Kampasi Kuu Morogoro, wakati 47 watatunukia Shahada za Uzamili kwenye Shule ya Biashara ya Mzumbe iliyopo Dar es Salaam Desemba 16, na 383 watatunukiwa shahada zao kwenye Kampasi ya Mzumbe Mbeya Desemba 10, mwaka huu.

MHAFALI YA 10, CHUO KIKUU MZUMBE

 

Mhitimu wa kozi ya Public Administration in Health Service Management, Enighenja Amiri akipata chakula mara baada ya kutunikiwa cheti chake.
..
Mmoja wa wahitimu akivalishwa taji na mmoja kati ya ndugu zake.
CHUO Kikuu cha Mzumbe, Morogoro jana kiliadhimisha mahafali ya 10 na wahitimu wa kozi tofauti waliweza kutunikiwa vyeti vyao.
 
Sherehe zikiendelea katika garden za chuo hicho.
Picha kwa hisani ya Global Publishers

PICHA ZOTE NA ERICK EVARIST/ GPL

Tuesday, November 22, 2011

Workshops zatumika kama forums za kampeni, siri yafichuka , wenye nia watumia kujitangaza

 Kile kitendawili cha baadhi ya workshops zinazofanyika Mzumbe University kukosa dhima kiasi cha wadau kuhoji kuwa zina faida gani? au zinamfaidisha nani? sasa kimeteguliwa baada ya Blog hii kujikusanyia ushahidi unaodhihirisha pasi na shaka wa baadhi ya workshops hizo kutumika kujenga mitandao ya kampeni. Blog hii imebaini jambo hili ikiwa ni takribani miezi miwili kabla ya uchaguzi mkuu wa MUSO ambao kadri muda unavyoenda na joto linazidi kupanda kwa kasi. Baadhi ya mbinu zinazotumika kujenga mitandao ya kampeni ni pamoja na wale wenye nia kupata wasaa wa kuzungumza hata kama hawana hoja za msingi lakini pia kumekuwa na tabia ya kukusanya namba za simu za wale wanaosadikiwa kuwa wapiga kura.

Breaking Newz; Waziri ataka wanafunzi waandamane kuwadai wenzao waliokopa walipe

http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2011/06/Philipo-Mulugo.jpg
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo
Peter Saramba, Arusha NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo amewasihi wanafunzi wa elimu ya juu nchini kuandamana ili kushinikiza waliokopeshwa fedha za elimu miaka ya nyuma walipe ili wapewe wengine. Amesema wahitimu wengi walikopeshwa zaidi ya Sh21 bilioni ili kusoma kwenye vyuo mbalimbali, lakini baada ya kupata kazi wanakwepa kulipa mikopo hiyo. Mlugo alisema wanaosoma vyuoni sasa hawana budi kuandamana ili kuwashinikiza waliotangulia walipe fedha hizo ili ziweze kukopeshwa kwa wanafunzi wengine zaidi.
“Fedha hizo zilikopeshwa kwa wanafunzi wa elimu ya juu tangu utoaji wa mikopo ulipoanza mwaka wa masomo wa 2004/05 na kama zitapatikana zitaiwezesha Serikali kukopesha wahitaji wengi zaidi kuliko idadi ya sasa”, alisisitiza. Naibu Waziri Mulugo alisema hayo alipozungumza kwenye sherehe za mahafali ya Saba ya Chuo Kikuu cha Mount Meru eneo la Ngaramtoni, nje kidogo ya mji wa Arusha. Alisema baadhi ya wanaodaiwa fedha hizi wamefanikiwa kupata ajira rasmi huku wengine wakijiajiri wenyewe baada ya Serikali kugharamia elimu yao kupitia mikopo ambayo sasa hawataki kurejesha. “Tusiandamane (wanafunzi) kudai mikopo kutoka bodi ya mikopo pekee, sasa tuandamane pia kushinikiza waliokopeshwa sasa wanafanya kazi au kujiajiri warejeshe fedha walizokopeshwa ili ziingizwe kwenye mzunguko utakaowezesha wengi kufaidika,” alisema Mulugo akipigiwa makofi. Alisema Serikali ina nia ya dhati kuhakikisha wote wanaofaulu na kupata sifa za kujiunga na elimu ya juu wanapata fursa hiyo bila kujali uwezo kiuchumi wa mhusika, wazazi au walezi wake, lakini lengo hilo linakwamishwa na kipato kidogo na changamoto nyingi zinazohitaji kushughulikiwa na Serikali akitaja uboreshaji wa huduma za afya, miundombinu na huduma zingine za kijamii. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Naibu waziri huyo, idadi ya wanafunzi wa elimu ya juu wanaokopeshwa imekuwa ikiongezeka kila mwaka wa masomo ambapo mwaka 2004/5 , Sh 9.9 bilioni zilitumika kuwakopesha wanafunzi 16,345 kabla ya idadi hiyo kuongezeka hadi kufikia wanafunzi 42,729 mwaka uliofuata. Kuhusu maendeleo katika sekta ya elimu, hasa elimu ya juu, Naibu waziri huyo alisema nchi ilipopata uhuru mwaka 1961 kulikuwa na chuo kikuu kimoja pekee lakini sasa vipo vyuo vikuu na vyuo vikuu vishiriki 41, kati ya hivyo 12 vikiwa vy umma na 29 vya binafsi huku udahili ukiongezeka kutoka wanafunzi 14 kwa wakati huo hadi 155,757 kwa sasa. Katika risala yao kwa mgeni rasmi, wahitimu 414 wa Chuo Kikuu cha Mount Meru waliishauri serikali kuwa pamoja na kuanzisha dawati la mikopo vyuoni, muda umefika wa kufikiria kuanzisha Ofisi za Kanda za Bodi ya Mikopo ili kurahisisha na kuongeza ufanisi kiutendaji.

Chanzo; Gazeti la Mwananchi

ST John Wafanya Mahafali

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhxxkNq50wi80kAU97af45J7jpDpzNLwRWEpsy7xq00U-0RDaX0OGnsgPAHbmntw-LiEJhvy2ZbIUzyOLvFZsbLH9kj2ksLLKHu34J3lJQ5TtBsc0p6OBL0STO2ETQjRUF9r_HzSncmwrYT/s640/IMG_7710.JPG
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akiwa na baadhi ya viongozi wa Chuo Kikuu cha
Mtakatifu Yohana (Saint John's University cha Dodoma katika mhafali ya
chuo hicho Novemba 5,2011. Kushoto kwake ni Mkuu wa Kanisa la Anglikan
nchini linalomiliki chuo hicho, Askofu, Dr. Valentino Mokiwa na kulia
kwake ni Mkuu wa Chuo hicho, Askofu Mstaafu, Dr. Donald Mtetemela.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Habari kwa hisani ya Blog ya wanavyuo Tanzania

Ms Asela Miho The pride of Mlimani

http://dailynews.co.tz/pics/11_11_gemg20.jpg
The
Chancellor of University of Dar es Salaam, Ambassador Fulgence Kazaura
(left) gives a reward to Ms Asela Miho (right) who graduated with a BA
degree and was the best overall student during the 4th graduation
ceremony of Dar es Salaam University College of Education (DUCE) on
Saturday. (Photo
by Yusuf Badi)

Monday, November 21, 2011

FIRST YEAR COLLEGE BASH 2011 @ NEW MAISHA CLUB


Mawazo gongana; Zamzam, Frank Mhilu &Lupakisyo Mwambinga


Zamzam anasema..."I appriciate t. Congrats to ministry of informtn, communication and technology. Rais umetendea haki wizara hii."


Lupakisyo Mwambinga anasema..."Huu utaratibu ulioanzishwa sikuhizi Green wa kutenganisha dirisha la watu wa msosi wa buku na dirisha la msosi ambao ni zaid ya buku kwa mtazamo wangu sijaupenda its like ubaguz fulani wa wateja na sisi ni wanafunzi."


Frank Mhilu anasema....ni dhahiri, maji mazito hayabebeki, hata pamba vilevile,...
 najiuliza hizi kelele za ufisadi wa muso mwisho wake lini, au tulete dr toka india, nadhani ifikie mahali tuseme basi inatosha, viongozi lazima tuwajibike, wadau tunapaswa pia kuwajibika

 safari hii hatuna masihara , tutawajibishana tu.

Sunday, November 20, 2011

Maoni ya Mhariri Leo; Acha Punch, acha Majungu, Lete Hoja Mezani

wabunge wa Mzumbe wakiwa Bungeni
Kwenu Wanamzumbe,
Naandika tahariri hii nikiwa na majonzi makubwa kwa jinsi baadhi ya Wanamzumbe wanavyotaka kutuvuruga kwa kile kinachoweza kutafsiriwa kuwa ni "tamaa ya madaraka". Ikiwa takribani ni miezi miwili kabla ya uchaguzi mkuu wa MUSO tayari kampeni za chini kwa chini zimeanza (ingawaje ni kinyume na sheria) nimeshalisema hili siwezi kurudia tena walionisikia wameelewa na ambao hawataki kuelewa wangoje sheria itakapowakumbusha wajibu wao. Leo najitokeza tena kulaani vikali "zengwe" miongoni mwa wanamzumbe.

Hapa neno zengwe ni kuchafuana ambapo kunaweza kutafsiriwa kama kupigana punch na majungu, naam! mapuynch na majungu hayawezi kukubalika hata kidogo. Kama wasomi hatulikubali hili , hatulitaki na tutalilaani milele. Sisi ni wasomi hivyo tutaendelea kusimama katika ukweli ndiyo maana nasema kuwa umefika wakati sasa kwa Wanamzumbe kuanza kujitafakari na kuchukua uamuzi sahihi badala ya kuendelea kukumbatia "siasa za majitaka" Naam! iwe isiwe nitasema ukweli daima, leo nasisitiza kuwa Acha punch, acha majungu, lete hoja mezani!

Wabunge Wanavyoipa heko Mzumbe University

Na Mwandishi wetu Dodoma,
Blog hii imefanikiwa kutua mjini Dodoma na kufahamu mbivu na mbichi kuhusu waheshimiwa wabunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania "kuifagilia" Mzumbe University kwa kile kinachodaiwa mafanikio ya kitaaluma , amani na utulivu wa chuo hiki huku wakichagiza "kwanini vyuo vingine visiige kutoka Mzumbe?"
Kutokana na hali hii, wataalamu wa maswala ya miradi na nertworking katika njanja za maendeleo na ujasiriamali chuoni hapa wanatoa wito kwa chuo kikuu Mzumbe kuitumia fursa hii kufanikisha agenda ya maendeleo huku wakisisitiza kuwa "Mzumbe must market its good reputation"