Friday, November 18, 2011

Prof Joseph Kuzilwa azungumza na Wanamzumbe kuhusu Changamoto zinazowakabili


Makamu mkuu wa Chuo kikuu Mzumbe Prof Joseph Kuzilwa amezungumza na wanafunzi wa chuo kikuu Mzumbe( mwaka wa pili) kuhusu kero zinazowakabili siku ya jana. Taarifa ambazo Blog hii imezipata ni kuwa hatua hiyo ya Prof Kuzilwa imefuatiwa na ombi la wanachuo hao hasa mwaka wa pili walioomba kuonana na mkuu huyo wa chuo ambaye pamoja na mambo mengine walieleza kero mbalimbali kubwa likiwa ni swala la mikopo kwa wanafunzi wa mwaka wa pili, ambapo pamoja na swala hilo pia swala la Accomodation lilizungumzwa kwa undani ikizingatiwa kuwa sasa utaratibu wa TCU wa kudahili maelfu ya wanafunzi kwenye vyuo vingi hauna maana kwa mantiki kuwa wanafunzi wanaodahiliwa wanazidi hata uwezo wa baadhi ya vyuo kutoa huduma ya malazi kwa wanafunzi. Katika utatuzi wa swala hilo la mikopo Prof Kuzilwa ameridhia chuo kuwapatia wanafunzi hao shilingi laki tatu na nusu kila mmoja mpaka pale Bodi ya mikopo itakapowapatia fedha zao, pia amesisitiza kuwa swala la accomodation linamnyima usingizi professor huyo.

No comments:

Post a Comment