Thursday, November 17, 2011

Fred Kanuti Valentino; Mwanamzumbe , Ndugu Yetu lala Mahali Pema Peponi!

Marehemu Fred Kanuti


Tarehe 26 mwezi wa 10 mwaka huu Jumuiya ya Wanamzumbe ilipatwa na majonzi mazito kama sio mtikisiko mkubwa kufuatia kuaga Dunia kwa mwanafunzi mwenzetu wa mwaka wa tatu ndugu yetu Fred Kanuti Valentino kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kansa ya damu, Blog hii ilikuwepo kwenye mazishi ya ndugu yetu huyu yaliyofanyika Kimara Temboni jijini Dar es salaam, fatilia picha zifuatazo ili uelewe kilichojiri....;

Mwili wa ndugu yetu Fred ukiwa kwenye jeneza tayari kwa kupewa heshima za mwisho

Watu wakitoa heshima za mwisho
Mama huyu akimlilia ndugu yetu Fred ilikuwa ni huzuni kubwa
Huyu ni Vice President wa MUSO Happiness Joseph akimlilia Fred
Baba Dean akiwa na huzuni kubwa

Hapa ilikuwa kanisani , Ibada ya mazishi ikiendelea

Jeneza likishushwa kaburini
Jeneza likiwa ndani ya kaburi
Msalaba ukiwekwa juu ya kaburi
Kaburi la ndugu yetu Fred likiwa limepambwa kwa maua na mishumaa kuashiria watu walivyompenda
Hapa ndipo alipolala mpendwa wetu Fred Kanuti Valentino.
KWA NIABA YA WANAFUNZI WA CHUO KIKUU MZUMBE BLOG HII INATOA POLE KWA NDUGU WA MAREHEMU, DAIMA TUTAMKUMBUKA FRED, AMEN!










No comments:

Post a Comment