Friday, November 18, 2011

Mh Amon Chakushemeire; Kajiuzulu au ameandika barua ya kuomba kujiuzulu?

Mh Chakushemeire akizungumza kwenye baraza la mawaziri 
Giza limetanda kufuatia taarifa za kujiuzulu kwa waziri wa Protocal wa MUSO Bw Amon Chakushemeire ambazo zimebaki kuwa "hazieleweki". Blog hii imefatilia kwa undani swala hilo na kubaini kuna uelewa mdogo wa mambo ya utawala miongoni mwa watu wanaoeneza taarifa hiyo kwa maana tunaomba tuweke wazi hapa kuwa alichofanya Mh Chakushemeire ni kuandika barua ya kuomba kujiuzulu kwa aliyemteua(rais) ambaye hata hivyo sheria zinamruhusu kuridhia ombi hilo au kukataa hivyo mpaka sasa bado rais wa MUSO hajatoa uamuzi wake kwa maana nyingine Mh Chakushemeire anapaswa kuendelea kuwajibika mpaka rais atakapotoa uamuzi wake vinginevyo kinachofanyika hapa ni kinyume cha sheria hivyo lazima lipingwe vikali nasi tunakuwa watu wa kwanza kutoa msimamo wetu juu ya hili kuwa HATUKUBALIANI NALO.

No comments:

Post a Comment