Sunday, November 13, 2011

Hoja yetu; Tatizo si Kampeni bali Muda Haujafika

Na Mhariri Mkuu,
Nianze na nukuu ya waziri mkuu wa MUSO Bw Benson Futte aliyowahi kuitoa wakati akizungumza bungeni aliwahi kunukuliwa akisema "uongozi na dhamana na hakika ni kazi kubwa inayohitaji kujitoa kuwatumikia watu" swadakta haya hakika ni maneno ya busara na hayakusemwa kimakosa ila kinachotusikitisha ni jinsi baadhi ya watu walivyoanza kampeni kabla ya muda. Ukirejea mtiririko wa mantiki tunayojenga hapa utabaini kuwa hatuwapingi wanaotaka uongozi , abadani hatupingi kampeni ila tunachosema ni kuwa TATIZO SI KAMPENI BALI MUDA HAUJAFIKA.

Tunayasema haya siyo kwa majungu bali tukiwa na uhakika wa zaidi ya asilimia mia moja kutokana na utafiti wa muda mrefu ambao umebaini kuwa kuna baadhi ya watu wenye lengo la kugombea urais wameanza kampeni kabla ya wakati hivyo tunachukua nafasi hii kuwakanya na kuwataka waache mara moja harakati hizo ambazo ni kinyume cha sheria badala yake tunawataka wangoje muda mwafaka.

No comments:

Post a Comment